• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • NeST |
    • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS)) |
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Huduma Zetu
    • Kikundi cha Bagamoyo
    • Vyumba vya Mikutano
    • Ushauri
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Ofisi
    • Vitengo
  • Taaluma
    • Kozi Zitolewazo
    • Fomu za Maombi
    • Matokeo ya Mtihani
    • Prospectus
  • Tamasha la Bagamoyo
    • Kuhusu Tamasha
    • Mwongozo wa Tamasha
    • Fomu za Maombi ya Tamasha
    • Tamasha la 43
    • Tamasha la 42
    • Tamasha la 41
    • Tamasha la 40
    • Tamasha la 39
    • Tamasha la 38
  • Kituo cha habari
    • TaSUBa TV
    • Maktaba ya Picha
  • Wasiliana
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Majarida
    • Vipeperushi
    • Taarifa kwa umma

Mchengerwa: Serikali Kuboresha Sekta ya Filamu Nchini

Posted on: April 9th, 2022

Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo imekuja na nguvu kubwa ili kuleta maboresho na mabadiliko ya kisasa katika ukuaji wa Sekta ya Filamu nchini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Mohammedi Mchengerwa alipotembelea Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) April 09, 2022.

Mhe. Waziri ambaye aliongozana Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Said Yakubu, pamoja na viongozi kutoka Kampuni ya Nichani ya India ikiongozwa na Bw. Manu Nichani na Trans Innova ya Marekani ikiongozwa na Dkt. David Faria, amesema lengo la kuja kwa viongozi hao ni kuona namna gani wanaweza kutusaidia kufanya mabadiliko ya pamoja na kupata uzoefu katika sekta ya filamu.

“Dhamira ya Serikali ni kuleta mapinduzi ya dhati katika Sekta ya Filamu na tumedhamiria kweli kweli kuitoa hapa ilipo na kuipeleka mbele zaidi,” alisema Mhe. Mchengerwa.

Mhe. Waziri amesema Wizara kupitia mashirikiano baina ya Kampuni hizo mbili itafanya mambo makubwa ambayo watanzania watayafurahia na yatadumu kwa kizazi cha leo na cha baadae.

Mhe. Waziri amesema, wataalam hao wanampango wa kukutana wa waigizaji wa filamu nchini ili nao wapate uzoefu wa namna ya kuzalisha filamu na tamthilia.

“Wenzetu hawa wametupa uhakika wa kutusaidia katika kupata masoko, kutangaza kazi zetu na kuzifanya ziwe za kimataifa zaidi, amesema Mhe. Mchengerwa.

Mhe. Mchengerwa amesema ziara hio ilikua muhimu kwasababu itakua na manufaa kwetu ili wenzetu hao waweze kutusaidia kutuvusha hapa tulipo na kwenda mbele zaidi.

Mhe. Waziri amesema kama nchi tunataka tuwe miongoni mwa mataifa ambayo yako mbele zaidi katika kuandaa filamu.

“Tutaendelea kuwatia moyo waandaaji wa filamu, waigizaji na wazalishaji wa filamu, lakini pia wanunuzi wa filamu ili kwa pamoja tuweze kufanikisha wazo na maono ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ambaye amedhamiria kuhakikisha Wizara hii inaleta furaha na faraja kwa Watanzania,” amesema Mhe. Waziri.

Naye Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt. Herbert Makoye amesema TaSUBa inapata nguvu kubwa ya kusonga mbele kutokana na ushirikiano na uwezeshwaji mkubwa ambao Chuo kinapata kutoka kwa Serikali kupitia Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo.

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA NA CHUO KWA MWAKA WA MASOMO 2025-2026 SEPTEMBER INTAKE May 28, 2025
  • JOIN INSTRUCTION KWA MWAKA WA MASOMO 2025/2026 April 02, 2025
  • Call for the artists Bagamoyo Festival - 2025 May 05, 2025
  • Wito kwa wasanii Tamasha la Bagamoyo - 2025 May 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KARIBU UJIUNGE NA KOZI YA MUDA MFUPI YA MUZIKI

    May 29, 2025
  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    March 04, 2025
  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    December 19, 2024
  • *SERIKALI KUENDELEA KUFANYA UWEKEZAJI MKUBWA TaSUBa*

    December 07, 2024
  • Angalia zote

Video

KARIBU JIUNGE NA CHUO TaSUBa KWA MUHULA WA MACHI 2025
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS))
  • Dirisha la Hati ya Mshahara
  • Baraza la Sanaa la Taifa

Viunganishi Linganifu

  • WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Kaole Road

    Anuani ya posta: P.O.BOX 32 Bagamoyo Tanzania

    Simu: +255 762544613

    Simu ya kiganjani: +255 766 264 581

    Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas

Other Contacts

   

Idadi ya waliotembelea Tovuti

Counter Widgets

    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.