• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • NeST |
    • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS)) |
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Huduma Zetu
    • Kikundi cha Bagamoyo
    • Vyumba vya Mikutano
    • Ushauri
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Ofisi
    • Vitengo
  • Taaluma
    • Kozi Zitolewazo
    • Fomu za Maombi
    • Matokeo ya Mtihani
    • Prospectus
  • Tamasha la Bagamoyo
    • Kuhusu Tamasha
    • Mwongozo wa Tamasha
    • Fomu za Maombi ya Tamasha
    • Tamasha la 43
    • Tamasha la 42
    • Tamasha la 41
    • Tamasha la 40
    • Tamasha la 39
    • Tamasha la 38
  • Kituo cha habari
    • TaSUBa TV
    • Maktaba ya Picha
  • Wasiliana
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Majarida
    • Vipeperushi
    • Taarifa kwa umma

*SERIKALI KUENDELEA KUFANYA UWEKEZAJI MKUBWA TaSUBa*

Posted on: December 7th, 2024



SERIKALI kupitia Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo itaendelea kufanya uwekezaji mkubwa katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ili kuendelea kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia kutokana na upekee wa Chuo hicho katika ukanda wa Afrika Mashariki.


Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo Bw. Gerson Msigwa katika Mahafali ya 35 ya Taasisi hiyo yaliyofanyika Chuoni Bagamoyo Desemba 06, 2024.


Msigwa amesema TaSUBa ndio Chuo pekee kinacho toa mafunzo ya sanaa kwa ngazi ya Astashahada na Stashahada hivyo kuwa na umuhimu mkubwa wa kuboresha zaidi taaluma inayotolewa Chuoni hapo ili iendane na kasi ya ukuaji wa matumizi ya teknolojia mpya katika uzalishaji wa kazi za sanaa hasa ugunduzi wa matumizi ya akili mnemba (AI)


“Nimeyasema hayo ili tuweze kuona namna Serikali ilivyojipanga kukifanya Chuo hiki kiweze kuzalisha wahitimu ambao tayari soko linawahitaji katika viwanda vya uzalishaji wa Sanaa ya Ubunifu,” amesema Msigwa.


Msigwa amesema ana matarajio makubwa kwa wahitimu kuwa, elimu waliyoipata itawasaidia kuingia kwenye tasnia ya sanaa na utamaduni wakiwa na mwelekeo wa sasa wa Serikali na Wizara wa kuzalisha ajira zaidi na kukuza biashara na uchumi kupitia kazi za sanaa.


“Kila mmoja wenu kwa nafasi yake anapaswa alijue hilo na abadilishe elimu na ujuzi alioupata ili kujiari na kuajiri wengine kufanya sanaa kwa mrengo wa biashara na kukuza uchumi wake na taifa kwa ujumla,” amesema Msigwa.


Katibu Mkuu Msigwa amewataka wahitimu na wasanii wote kuzingatia maadili ya Taifa hasa wanapozalisha kazi za sanaa na watambue kuwa wao ni kioo cha jamii. 


Msigwa ameitaka TaSUBa kuendelea kutoa mafunzo ya muda mfupi na kozi maalumu kwa wasanii na viongozi wa mashirikisho ya sanaa na vyama vya wasanii nchini ili kuendeleza vipaji vyao kwa pamoja.





Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA NA CHUO KWA MWAKA WA MASOMO 2025-2026 SEPTEMBER INTAKE May 28, 2025
  • JOIN INSTRUCTION KWA MWAKA WA MASOMO 2025/2026 April 02, 2025
  • Call for the artists Bagamoyo Festival - 2025 May 05, 2025
  • Wito kwa wasanii Tamasha la Bagamoyo - 2025 May 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KARIBU UJIUNGE NA KOZI YA MUDA MFUPI YA MUZIKI

    May 29, 2025
  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    March 04, 2025
  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    December 19, 2024
  • *SERIKALI KUENDELEA KUFANYA UWEKEZAJI MKUBWA TaSUBa*

    December 07, 2024
  • Angalia zote

Video

KARIBU JIUNGE NA CHUO TaSUBa KWA MUHULA WA MACHI 2025
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS))
  • Dirisha la Hati ya Mshahara
  • Baraza la Sanaa la Taifa

Viunganishi Linganifu

  • WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Kaole Road

    Anuani ya posta: P.O.BOX 32 Bagamoyo Tanzania

    Simu: +255 762544613

    Simu ya kiganjani: +255 766 264 581

    Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas

Other Contacts

   

Idadi ya waliotembelea Tovuti

Counter Widgets

    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.