• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • NeST |
    • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS)) |
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Huduma Zetu
    • Kikundi cha Bagamoyo
    • Vyumba vya Mikutano
    • Ushauri
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Ofisi
    • Vitengo
  • Taaluma
    • Kozi Zitolewazo
    • Fomu za Maombi
    • Matokeo ya Mtihani
    • Prospectus
  • Tamasha la Bagamoyo
    • Kuhusu Tamasha
    • Mwongozo wa Tamasha
    • Fomu za Maombi ya Tamasha
    • Tamasha la 43
    • Tamasha la 42
    • Tamasha la 41
    • Tamasha la 40
    • Tamasha la 39
    • Tamasha la 38
  • Kituo cha habari
    • TaSUBa TV
    • Maktaba ya Picha
  • Wasiliana
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Majarida
    • Vipeperushi
    • Taarifa kwa umma

*SANAA ITUMIKE KUWAUNGANISHA WATANZANIA BILA KUJALI TOFAUTI ZAO*

Posted on: October 29th, 2023

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko amefunga Tamasha la 42 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo akisisitiza kuwa Sanaa ina uwezo mkubwa wa kuwaunganisha Watanzania bila kujali tofauti za kabila, dini na maeneo wanayotoka.

Akimwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika hafla ya kufunga tamasha hilo Oktoba 28, 2023 mjini Bagamoyo, Dkt. Biteko amewasihi wasanii wote nchini watengeneze kazi za Sanaa zinazohimiza watu kupenda utu na kufanya kazi ili kuendeleza kujenga taifa lenye taswira njema linalotambuliwa kwa utamaduni wake.

“Ninyi Wasanii wa Tanzania, kwa kushirikiana na taasisi yetu hiii ya Sanaa Bagamoyo endeleeni kutengeneza kazi za Sanaa zinazojenga umoja na uzalendo, kuhimiza Watanzania kupenda kazi ambayo ni kipimo cha Utu” amesema Dkt. Biteko.

Kwa upande wake Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye ambaye alimwakilisha Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Damas Ndumbaro amesema Tamasha hilo limekuwa kwa matokeo mzuri na wananchi wanajitokeza kwa wingi kwa kuzingatia linasimamiwa na Wizara ya furaha na wananchi wataendelea kupata burudani kupitia kazi za Sanaa na michezo.

Naye Mkuu wa mkoa wa Pwani Bw. Abubakari Kunenge amesema mkoa huo umejipanga vizuri na mazingira ya mkoa huo ni usalama, yapo vizuri na amewahakikishia washiriki usalama wao wakati wote wa tamasha hilo akiwakaribisha watembelee maeneo yote ya mji ya kihistoria ya Bagamoyo ambayo yamesheheni historia na vivutio lukuki vya utalii.

Tamasha hilo limehusisha maonesho ya sanaa za jukwaani ikiwemo ngoma za asili na za kisasa, muziki wa asili na wa kisasa, maigizo, sarakasi, ushairi, vichekesho na mazingaombwe kutoka Tanzania na vikundi vya Kimataifa kutoka nchi za Canada, Botswana, Afrika Kusini, Uganda, Zambia, Burundi, na Kenya.

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA NA CHUO KWA MWAKA WA MASOMO 2025-2026 SEPTEMBER INTAKE May 28, 2025
  • JOIN INSTRUCTION KWA MWAKA WA MASOMO 2025/2026 April 02, 2025
  • Call for the artists Bagamoyo Festival - 2025 May 05, 2025
  • Wito kwa wasanii Tamasha la Bagamoyo - 2025 May 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KARIBU UJIUNGE NA KOZI YA MUDA MFUPI YA MUZIKI

    May 29, 2025
  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    March 04, 2025
  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    December 19, 2024
  • *SERIKALI KUENDELEA KUFANYA UWEKEZAJI MKUBWA TaSUBa*

    December 07, 2024
  • Angalia zote

Video

KARIBU JIUNGE NA CHUO TaSUBa KWA MUHULA WA MACHI 2025
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS))
  • Dirisha la Hati ya Mshahara
  • Baraza la Sanaa la Taifa

Viunganishi Linganifu

  • WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Kaole Road

    Anuani ya posta: P.O.BOX 32 Bagamoyo Tanzania

    Simu: +255 762544613

    Simu ya kiganjani: +255 766 264 581

    Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas

Other Contacts

   

Idadi ya waliotembelea Tovuti

Counter Widgets

    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.