• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • NeST |
    • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS)) |
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Huduma Zetu
    • Kikundi cha Bagamoyo
    • Vyumba vya Mikutano
    • Ushauri
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Ofisi
    • Vitengo
  • Taaluma
    • Kozi Zitolewazo
    • Fomu za Maombi
    • Matokeo ya Mtihani
    • Prospectus
  • Tamasha la Bagamoyo
    • Kuhusu Tamasha
    • Mwongozo wa Tamasha
    • Fomu za Maombi ya Tamasha
    • Tamasha la 43
    • Tamasha la 42
    • Tamasha la 41
    • Tamasha la 40
    • Tamasha la 39
    • Tamasha la 38
  • Kituo cha habari
    • TaSUBa TV
    • Maktaba ya Picha
  • Wasiliana
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Majarida
    • Vipeperushi
    • Taarifa kwa umma

TaSUBa YAENDESHA KAMPENI YA ELIMU KUHUSU MADHARA YA MIMBA ZA UTOTONI NA UMUHIMU WA ELIMU KWA MABINTI

Posted on: May 16th, 2022

Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kwa kushirikiana na Taasisi ya Bagamoyo Friendship Society ya Ujerumani imeendelea na kampeni yake ya kutoa elimu katika vijiji vya Msata na Msoga Wilayani Chalinze kuhusu athari za mimba za utotoni ambazo ni changamoto kubwa kwa ustawi wa mtoto wa kike.  

Kampeni hii ambayo inafanyika katika baadhi ya Vijiji vya Wilaya za Bagamoyo na Chalinze imekua ya mafanikio makubwa kutokana na muitikio wa kuridhisha kutoka kwa wananchi kwa kuhudhiria kampeni hizo.

Kampeni imeanza Mei 06, 2022 na inafanyika kupitia sanaa shirikishi au sanaa kwa maendeleo ya jamii kwa mtindo wa igizo ambapo itadumu kwa muda wa kipindi cha wiki tatu.

Sanaa shirikishi ni tofauti na sanaa zingine za jukwaani ambazo zinakua ni za kufikirika tu. Sanaa shirikishi inaanza kwa hatua ya utafiti wa matatizo kwenye jamii husika, matatizo hayo yakibainika kutengenezewa sanaa kwa ajili ya kuielimisha jamii hiyo.

Aidha wananchi waliohudhuria kampeni hiyo baada ya igizo walipata fursa kupitia tafakuri ya sanaa waliyoiona kubainisha sababu za wasichana kupata ujauzito katika umri mdogo, changamoto zinazojitokeza baada ya mtoto kupata mimba na nini kifanyike ili kuepukana na changamoto hii.

Baadhi ya sababu za mimba za utotoni zilizotajwa ni mazingira magumu ya upataji wa elimu kwa mtoto wa kike mfano wanafunzi kutembea umbali mrefu kwenda shuleni, kuishi mtaani kutokana na ukosefu au upungufu wa hosteli, mila na desturi ya kuwacheza ngoma watoto wa kike kabla hawajamaliza shule, wahalifu kuendelea kuwepo mtaani kutokana na mashauri kumalizwa kienyeji, umaskini ambao huwafanya watoto wa kike waingie katika tamaa ya fedha, wazazi kutofuatilia maendeleo ya watoto shuleni, wasichana kutopata elimu ya jinsia na mahusiano, mmomonyoko wa maadili katika familia na jamii kwa ujumla.

Changamoto anazokutana nazo binti baada ya kupata ujauzito zilitajwa kuwa ni matatizo wakati wa kujifungua ambapo wakati mwingine hupelekea vifo kwa mama au/na mtoto, kufukuzwa nyumbani na wazazi, ongezeko la watoto wa mtaani, mtoto kushindwa kuendelea na masomo hivyo ndoto zake kukoma.

Wananchi hao walitoa suluhu kwa changamoto hizo kuwa ni pamoja na wazazi kuongea na watoto kuhusu mabadiliko ya miili yao, mabinti kutopewa uhuru uliopitiliza, elimu ya jinsia na mahusiano itolewe mashuleni, watoto wa kike wajengewe hosteli eneo la shuleni, sheria zisimamiwe kikamilifu, watekelezaji wa kadhia hiyo wapewe kifungo na adhabu kali, watoto wakishajifungua wapewe nafasi ya kurudi shuleni kumalizia masomo yao.

Mimba za utotoni imekuwa ni changamoto kubwa nchini, husani katika maeneo ya vijijini. Serikali ikishirikiana na wadau mbalimbali wa elimu, ustawi wa jamii, mashirika ya kitaifa na kimataifa inafanya jitihada kumkwamua mtoto wa kike katika changamoto hio kwa kuielimisha jamii wakiwemo wasichana wadogo mashuleni kuhusu athari za mimba hizo.

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA NA CHUO KWA MWAKA WA MASOMO 2025-2026 SEPTEMBER INTAKE May 28, 2025
  • JOIN INSTRUCTION KWA MWAKA WA MASOMO 2025/2026 April 02, 2025
  • Call for the artists Bagamoyo Festival - 2025 May 05, 2025
  • Wito kwa wasanii Tamasha la Bagamoyo - 2025 May 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KARIBU UJIUNGE NA KOZI YA MUDA MFUPI YA MUZIKI

    May 29, 2025
  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    March 04, 2025
  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    December 19, 2024
  • *SERIKALI KUENDELEA KUFANYA UWEKEZAJI MKUBWA TaSUBa*

    December 07, 2024
  • Angalia zote

Video

KARIBU JIUNGE NA CHUO TaSUBa KWA MUHULA WA MACHI 2025
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS))
  • Dirisha la Hati ya Mshahara
  • Baraza la Sanaa la Taifa

Viunganishi Linganifu

  • WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Kaole Road

    Anuani ya posta: P.O.BOX 32 Bagamoyo Tanzania

    Simu: +255 762544613

    Simu ya kiganjani: +255 766 264 581

    Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas

Other Contacts

   

Idadi ya waliotembelea Tovuti

Counter Widgets

    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.