• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • NeST |
    • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS)) |
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Huduma Zetu
    • Kikundi cha Bagamoyo
    • Vyumba vya Mikutano
    • Ushauri
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Ofisi
    • Vitengo
  • Taaluma
    • Kozi Zitolewazo
    • Fomu za Maombi
    • Matokeo ya Mtihani
    • Prospectus
  • Tamasha la Bagamoyo
    • Kuhusu Tamasha
    • Mwongozo wa Tamasha
    • Fomu za Maombi ya Tamasha
    • Tamasha la 43
    • Tamasha la 42
    • Tamasha la 41
    • Tamasha la 40
    • Tamasha la 39
    • Tamasha la 38
  • Kituo cha habari
    • TaSUBa TV
    • Maktaba ya Picha
  • Wasiliana
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Majarida
    • Vipeperushi
    • Taarifa kwa umma

TaSUBa YAZINDUA DAWATI LA JINSIA

Posted on: May 17th, 2023

TAASISI ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) leo Mei 17, 2023 imezindua dawati la jinsia ili  kutimiza malengo ya Serikali ya kupunguza na kumaliza kabisa  vitendo vya ukatili wa kijinsia  katika vyuo na jamii yote nchini.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Dawati hilo Mwenyekiti wa Kampeni ya Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania (SMAUJATA) Bi. Irene Mashine ambae ndiye alikua mgeni rasmi amesema, hivi sasa kumekuwa na ongezeko kubwa la matukio yanayohusiana na unyanyasaji wa kijinsia na mashambulio ya aibu ambayo mengine yanahusisha hata wanafamilia.

Bi. Mashine amewataka wajumbe wa dawati kutunza siri na kutoa msaada unaostahili kwa waathiriwa wa unyanyasaji huo ili kujenga jamii iliyo bora.

"Dawati hili la jinsia  liwe chachu katika kutokomeza ukatili wa  kijinsia hapa chuoni na sehemu zingine," amesema Bi. Mashine.

Naye Kaimu Mkuu wa Chuo Bw. Gabriel Kiiza amesema uzinduzi wa Dawati la Jinsia kwa TaSUBa ni wa umuhimu mkubwa kwa sababu litatoa muongozo nini kifanyike kukomesha vitendo hivyo kulingana na miongozo ya Serikali.

"Hivyo sisi kuzindua dawati hili, inatupa nafasi kubwa ya kuendelea kuwahimiza vijana kuepuka matendo yanayoashiria ukatili wa kijinsia," amesema Bw. Kiiza.

Mwenyekiti wa dawati hilo Bi. Perpetual Katondo amezitaja njia zitakazotumika kupata taarifa za unyanyasaji wa kijinsia kuwa ni pamoja na mlengwa au mtu aliyeshuhudia ukatili kufika moja kwa moja kwenye ofisi za dawati, kupiga simu kupitia namba ya wazi ambayo mtu yeyote anaweza kupiga na kutoa taarifa au kwa njia ya sanduku la maoni.

Hatua ya uzinduzi wa dawati hilo ni utekelezaji wa agizo la Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wanawake na Makundi Maalum kwa lengo la dawati kuwa na majukumu ya kutokomeza aina zote za ukatili maeneo ya vyuo.

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA NA CHUO KWA MWAKA WA MASOMO 2025-2026 SEPTEMBER INTAKE May 28, 2025
  • JOIN INSTRUCTION KWA MWAKA WA MASOMO 2025/2026 April 02, 2025
  • Call for the artists Bagamoyo Festival - 2025 May 05, 2025
  • Wito kwa wasanii Tamasha la Bagamoyo - 2025 May 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KARIBU UJIUNGE NA KOZI YA MUDA MFUPI YA MUZIKI

    May 29, 2025
  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    March 04, 2025
  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    December 19, 2024
  • *SERIKALI KUENDELEA KUFANYA UWEKEZAJI MKUBWA TaSUBa*

    December 07, 2024
  • Angalia zote

Video

KARIBU JIUNGE NA CHUO TaSUBa KWA MUHULA WA MACHI 2025
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS))
  • Dirisha la Hati ya Mshahara
  • Baraza la Sanaa la Taifa

Viunganishi Linganifu

  • WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Kaole Road

    Anuani ya posta: P.O.BOX 32 Bagamoyo Tanzania

    Simu: +255 762544613

    Simu ya kiganjani: +255 766 264 581

    Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas

Other Contacts

   

Idadi ya waliotembelea Tovuti

Counter Widgets

    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.