• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania WIZARA YA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Huduma Zetu
    • Kikundi cha Bagamoyo
    • Vyumba vya Mikutano
    • Ushauri
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Ofisi
    • Vitengo
  • Taaluma
    • Kozi Zitolewazo
    • Fomu za Maombi
    • Matokeo ya Mtihani
  • Tamasha la Bagamoyo
    • Kuhusu Tamasha
    • Mwongozo wa Tamasha
    • Fomu za Maombi ya Tamasha
    • Tamasha la 42
    • Tamasha la 41
    • Tamasha la 40
    • Tamasha la 39
    • Tamasha la 38
  • Kituo cha habari
    • TaSUBa TV
    • Maktaba ya Picha
  • Wasiliana
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Majarida
    • Vipeperushi
    • Taarifa kwa umma

KAMATI YA BUNGE YAPONGEZA TaSUBa KWA KUZALISHA WATAALAM MAHIRI WA SANAA NA UTAMADUNI

Posted on: March 18th, 2023

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo chini ya  Mwenyekiti wake Mhe. Prof. Kitila Mkumbo  imeipongeza Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa)  kwa  kufanya ukarabati wa miundombinu na kununua vifaa vya kufundishia na kujifunzia kama ilivyoelekezwa na Serikali.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Prof. Kitila Mkumbo ameyasema hayo wilayani Bagamoyo wakati Kamati hiyo ilipotembelea TaSUBa Machi 18, 2023 ili kukagua utekelezaji  wa Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2021/22 pamoja na kuona shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na Taasisi hiyo.

"Sekta ya Utamaduni na Sanaa inatoa ajira kwa watu wengi, ni vizuri tukaendelea kuwekeza na kuweka mazingira bora kwa Taasisi hii  ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya kutosha na ununuzi wa vifaa vya kisasa ili wadau wetu wapate mafunzo bora ya kuendeleza vipaji vyao," amesisitiza Mhe. Kitila.

Ameongeza kuwa ipo haja kwa Serikali kuiongezea  Bajeti Taasisi hiyo ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi pamoja na kuiongezea vifaa zaidi vya kujifunzia na kufundishia.

Kwa upande wao Wajumbe wa Kamati hiyo wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa ziara hiyo wametoa wito kwa wadau katika Sekta Binafsi hususani wasanii na wanufaika wa kazi za sanaa waendelee kujitokeza kuchangia maendeleo ya Taasisi hiyo kwa kujenga miundombinu na kutoa vifaa vya  kufundishia na kujifunzia badala ya kuiachia Serikali peke yake.

Naye Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana ameieleza Kamati hiyo kuwa Serikali inaeendelea kuweka jitihada kuboresha miundombinu ya Taasisi hiyo na inaialika Sekta binafsi pamoja na wadau wa sanaa kushirikiana na Serikali katika kukiendeleza Chuo hicho muhimu katika Sekta ya Sanaa na Utamaduni nchini.

Matangazo

  • JOIN INSTRUCTION FOR ACADEMIC YEAR 2023-2024 August 16, 2023
  • LIST OF SELECTED APPLICANTS FOR 2023 SEPTEMBER INTAKE August 21, 2023
  • FOMU YA KUJIUNGA NA CHUO KWA MWAKA WA MASOMO 2023-2024 (SECOND ROUND) August 16, 2023
  • WITO KWA WASANII KUSHIRIKI TAMASHA LA 42 LA KIMATAIFA LA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO -2023 April 20, 2023
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • IMEBAKI MWEZI MOJA KUFANYIKA TAMASHA LA 42 LA KIMATAIFA LA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO

    September 26, 2023
  • PONGEZI KWA KATIBU MKUU MPYA WA WIZARA

    September 23, 2023
  • TaSUBa YAZINDUA DAWATI LA JINSIA

    May 17, 2023
  • TaSUBa YASHIRIKI SHEREHE ZA MEI MOSI KIMKOA

    May 01, 2023
  • Angalia zote

Video

Sanaa Tuition fee waiver scholarship
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Sanaa la Taifa
  • Dirisha la Hati ya Mshahara
  • Dirisha la Watumishi

Viunganishi Linganifu

  • WIZARA YA UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Kaole Road

    Anuani ya posta: P.O.Box 32 Bagamoyo Tanzania

    Simu: +255 023 2440149

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas

Other Contacts

   

Idadi ya waliotembelea Tovuti

Counter Widgets

    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Copyright ©2022 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.