• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania WIZARA YA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Huduma Zetu
    • Kikundi cha Bagamoyo
    • Vyumba vya Mikutano
    • Ushauri
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Ofisi
    • Vitengo
  • Taaluma
    • Kozi Zitolewazo
    • Fomu za Maombi
    • Matokeo ya Mtihani
  • Tamasha la Bagamoyo
    • Kuhusu Tamasha
    • Tamasha la 41
    • Fomu za Maombi ya Tamasha
    • Tamasha la 40
    • Tamasha la 39
    • Tamasha la 38
  • Kituo cha habari
    • TaSUBa TV
    • Maktaba ya Picha
  • Wasiliana
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Majarida
    • Vipeperushi
    • Taarifa kwa umma

NAIBU WAZIRI GEKUL AIPONGEZA TaSUBa KWA USIMAMIZI MZURI WA RASILIMALI FEDHA PAMOJA NA KUWEKA HISTORIA YA UDAHILI MKUBWA

Posted on: December 1st, 2022

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Pauline Gekul ameupongeza uongozi wa Taasisi ya Sanaa na utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kwa usimamizi mzuri wa fedha zinazoletwa katika Taasisi hiyo kwa kuzitumia vyema kuendana na mahitaji ya taasisi ili kuifanya taasisi kufikia malengo yake.


Naibu Waziri Gekul ametoa pongezi hizo leo Desemba Mosi, 2022 akiwa ni mgeni rasmi katika mahafali ya 33 ya TaSUBa yaliyofanyika katika kampasi ya TaSUBa Bagamoyo mkoani Pwani na kusisitiza kuwa, taaluma ya utamaduni na sanaa inayotolewa chuoni hapo ni taaluma muhimu sana kwa maendeleo ya jamii yoyote duniani.


Mbali na hilo, pia ameipongeza TaSUBa kwa ongezeko kubwa la udahili wa Wanafunzi katika chuo hicho hata kufikia hatua ya kuweka historia ya kudahili idadi kubwa ya wanafunzi ambayo haijawahi kufikiwa tangu kuanzishwa kwa taasisi hiyo.


Kufuatia hilo naibu waziri Gekul amebainisha kuwa, serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan iliona wazi umuhimu wa taaluma hiyo na hivyo kuanzisha sera maalum kusimamia.


"TaSUBa ni taasisi ya pekee nchini kwetu na ukanda wa Afrika Mashariki inayotoa mafunzo ya sanaa kwa ngazi ya stashahada na astashahada hivyo basi kuna umuhimu mkubwa wa kuboresha taaluma hii ili iendane na mazingira ya sasa ya utandawazi"


Naibu Waziri huyo ameutaka uongozi wa TaSUBa kuendeleza ubunifu zaidi kwa kuanzisha kozi ambazo zitawavutia watu wengi kujiunga na chuo hicho.


Naye Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa), Dkt. Herbert Makoye amesema kuwa, kwa miaka mitatu mfululizo kumekuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi chuoni hapo na hiyo ni kutokana na jitihada mbalimbali zilizochuliwa na serikali ya awamu ya sita, wadau pamoja na wao wenyewe kama taasisi.


Dkt. Makoye amezitaja miongoni mwa jitihada hizo ni pamoja na uamuzi wa serikali kuwapangia wahitimu wa kidato cha nne moja kwa moja kujiunga na chuo hicho pamoja na uhamishaji wa kila siku unaofanywa na TaSUBa pamoja na wadau wengine katika kukitangaza chuo hicho.


#TaSUBaKwaMafunzoBoraYaSanaaNaUtamaduni

Matangazo

  • STUDENTS SELECTED MARCH INTAKE 2023 March 23, 2023
  • JOINING INSTRUCTION FOR MARCH INTAKE 2023 March 23, 2023
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA BUNGE YAPONGEZA TaSUBa KWA KUZALISHA WATAALAM MAHIRI WA SANAA NA UTAMADUNI

    March 18, 2023
  • SERIKALI KUENDELEA KUIBORESHA TAASISI YA SANAA - BAGAMOYO

    March 15, 2023
  • UDAHILI UMEFUNGULIWA MACHI INTAKE

    February 08, 2023
  • NAIBU WAZIRI GEKUL AIPONGEZA TaSUBa KWA USIMAMIZI MZURI WA RASILIMALI FEDHA PAMOJA NA KUWEKA HISTORIA YA UDAHILI MKUBWA

    December 01, 2022
  • Angalia zote

Video

Sanaa Tuition fee waiver scholarship
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Sanaa la Taifa
  • Dirisha la Hati ya Mshahara
  • Dirisha la Watumishi

Viunganishi Linganifu

  • WIZARA YA UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Kaole Road

    Anuani ya posta: P.O.Box 32 Bagamoyo Tanzania

    Simu: +255 023 2440149

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas

Other Contacts

   

Idadi ya waliotembelea Tovuti

Counter Widgets

    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Copyright ©2022 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.