• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania WIZARA YA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Huduma Zetu
    • Kikundi cha Bagamoyo
    • Vyumba vya Mikutano
    • Ushauri
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Ofisi
    • Vitengo
  • Taaluma
    • Kozi Zitolewazo
    • Fomu za Maombi
    • Matokeo ya Mtihani
  • Tamasha la Bagamoyo
    • Kuhusu Tamasha
    • Tamasha la 41
    • Fomu za Maombi ya Tamasha
    • Tamasha la 40
    • Tamasha la 39
    • Tamasha la 38
  • Kituo cha habari
    • TaSUBa TV
    • Maktaba ya Picha
  • Wasiliana
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Majarida
    • Vipeperushi
    • Taarifa kwa umma

Kuhusu Tamasha

Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni la Bagamoyo hufanyika kila mwaka mwezi Oktoba katika mji mkongwe na wa kihostoria wa Bagamoyo - mji wenye historia adhimu na vivutio lukuki vya urithi wa utamaduni wa Mtanzania vinavyotambuliwa na Shirika la UNESCO. Tamasha hili huandaliwa na kuendeshwa na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa); Taasisi inayotoa mafunzo ya sanaa na utamaduni kwa vijana wenye vipaji. Wakati wote wa Tamasha, maeneo yote ya TaSUBa hupambwa na kazi za sanaa na maonesho mbalimbali ya sanaa. Wasanii mahiri kutoka sehemu mbalimbali za Dunia ambao hufika kuonesha kazi zao za ubunifu wa hali ya juu. Aidha, Tamasha hili huvutia watazamaji, wadau na wapenzi wa sanaa kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje yaTanzania.

Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni la Bagamoyo lilianza mwaka 1981 kwa kushirikisha kazi za sanaa za wanafunzi na walimu wa TaSUBa pekee. Hata hivyo limeendelea kukua na kuwa maarufu sana na kuchukua sura ya Kitaifa kiasi cha kuwavutia watazamaji na wasanii wengi kutoka mataifa mbalimbali, hivyo kulifanya liwe la Kimataifa zaidi. Zaidi ya vikundi vya sanaa/ wasanii 1,500 wamepata nafasi ya kushiriki kwenye Tamasha hili tangu lianze; kati ya hawa, vikundi vya sanaa/ wasanii 1,300 wakiwa ni wa ndani na 200 ni kutoka nchi mbalimbali. Tamasha hili pia limekuwa kivutio kikubwa kwa watazamaji vijana kutoka katika shule na vyuo mbalimbali vya hapa nchini.

 

Lengo kuu la Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni la Bagamoyo ni kutoa nafasi kwa wasanii wa ndani ya nchi na wale kutoka nje kukutana na kusherehekea uanuai wa utamaduni unaochagiza mshikamano na bunifu mbalimbali. Malengo mahsusi ya Tamasha ni haya yafuatayo:

  • Kutoa nafasi kwa wanachuo wa TaSUBa na vyuo vingine kuonyesha kazi zao za sanaa ili kudhihirisha stadi au ujuzi waliopata kutokana na mafunzo ya taaluma ya sanaa na utamaduni.
  • Kutoa fursa kwa wasanii wa ndani na nje ya nchi kukutaana na kujenga mahusiano ya uendeshaji wa kazi za kisanii na utamaduni na kusherehekea uanuai katika Nyanja mbalimbali za sanaa na utamaduni.
  • Kutoa nafasi kwa wasanii vijana kuonyesha vipaji vyao kupitia njia ya sanaa.
  • Kuonyesha na kutangaza sanaa na utamaduni wa nchi zinazounda Jumuiya ya Afrika mashariki.
  • Kutoa nafasi kwa wasanii hasa vijana kuweza kukutana, kubasilishana uzoefu katika kukuza vipaji vyao vya sanaa na utamaduni.

Mbali na kukusanya wasanii maarufu wa ndani na nje, Tamasha hili hutoa nafasi ya kuonyesha sanaa za ufundi na vifaa vingine vya kiutamaduni, vyakula vya asili, kutembelea vivutio vya kitalii nchini Tanzania, michezo ya watoto na mafunzo mafupi mafupi ya utengenezaji au uandaaji wa sanaa.

  

Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo huandaliwa na:

Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa)

Barabara ya Kaole, S. L. P 32, Bagamoyo, Tanzanaia

Barua Pepe: info@tasuba.ac.tz/ tasuba@michezo.go.tz Wavuti: www.tasuba.ac.tz


Kuhusu Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni la Bagamoyo.p.pdf

Matangazo

  • STUDENTS SELECTED MARCH INTAKE 2023 March 23, 2023
  • JOINING INSTRUCTION FOR MARCH INTAKE 2023 March 23, 2023
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA BUNGE YAPONGEZA TaSUBa KWA KUZALISHA WATAALAM MAHIRI WA SANAA NA UTAMADUNI

    March 18, 2023
  • SERIKALI KUENDELEA KUIBORESHA TAASISI YA SANAA - BAGAMOYO

    March 15, 2023
  • UDAHILI UMEFUNGULIWA MACHI INTAKE

    February 08, 2023
  • NAIBU WAZIRI GEKUL AIPONGEZA TaSUBa KWA USIMAMIZI MZURI WA RASILIMALI FEDHA PAMOJA NA KUWEKA HISTORIA YA UDAHILI MKUBWA

    December 01, 2022
  • Angalia zote

Video

Sanaa Tuition fee waiver scholarship
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Sanaa la Taifa
  • Dirisha la Hati ya Mshahara
  • Dirisha la Watumishi

Viunganishi Linganifu

  • WIZARA YA UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Kaole Road

    Anuani ya posta: P.O.Box 32 Bagamoyo Tanzania

    Simu: +255 023 2440149

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas

Other Contacts

   

Idadi ya waliotembelea Tovuti

Counter Widgets

    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Copyright ©2022 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.