BAADHI ya wasanii wa timu ya waigizaji wa Tamthilia ya Kombolela wametembelea Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kwa lengo la kuwapa wanafunzi uzoefu kwa vitendo kuhusu kazi za sanaa nje ya mazingira ya darasani.
Akizungumza katika ziara hiyo iliyofanyika Februari 05, 2026, Mkuu wa Chuo Dkt. Herbert Makoye amesema ziara ya wasanii hao ni sehemu ya mikakati ya TaSUBa ya kuwajengea wanafunzi uwezo wa ubunifu na umahiri wa kitaaluma ili kuandaa wasanii wanaoweza kujiajiri na kuchangia maendeleo ya nchi yao kupitia kazi za sanaa.
"TaSUBa itaendelea kushirikiana na wasanii wenye uzoefu katika tasnia hii ya sanaa ili kuimarisha mafunzo yanayozingatia weledi kwa vitendo katika kuwapika vijana na kutoa wasanii bora," amesema Dkt. Makoye.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Bw. Lumole Matovolwa ambae ni mmoja wa wasanii wa Timu Kombolela amesema sanaa ina mchango mkubwa katika kufikisha ujumbe kwa jamii moja kwa moja, hususan katika masuala ya kijamii kama afya, elimu, uwajibikaji, mazingira na mshikamano katika jamii.
"Kupitia sanaa hii jamii hujifunza kwa njia rahisi na yenye kuvutia kwa kuwa inakua ni sehemu ya burudani," amesema Matovolwa.
Akiongea kwa ni niaba ya wakufunzi wa TaSUBa Bi. Beatrice Taisamo amesema ziara hiyo ni muhimu kwa wanafunzi kwani imewawezesha kujifunza kwa vitendo nje ya mazingira ya darasani na kuelewa uhalisia wa kazi ya sanaa katika jamii.
Naye mmoja wa wanafunzi wa TaSUBa Bi. Faraja Ibrahimu amesema ziara hiyo imewapanua mawazo na kuwajengea ujasiri wa kutumia sanaa kama chombo cha kuelimisha na kuhamasisha jamii.
Kaole Road
Anuani ya posta: P.O.BOX 32 Bagamoyo Tanzania
Simu: +255 762544613
Simu ya kiganjani: +255 766 264 581
Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas
Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.