Mkuu wa Chuo cha Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa), Dkt. Herbert Makoye, amesema kuwa TaSUBa Awards zimeanzishwa kwa lengo la kuwapa hamasa wanachuo ili wafanye vizuri zaidi katika masomo yao na kuendeleza vipaji vyao vya kisanii.Akizungumza kuelekea msimu wa tatu wa TaSUBa Awards, Dkt. Makoye alisema tuzo hizo ni sehemu ya kutambua juhudi, ubunifu na mafanikio ya wanafunzi katika nyanja mbalimbali za sanaa na utamaduni.“TaSUBa Awards ni tuzo zinazotoa hamasa kwa wanachuo wetu ili waweze kufanya vizuri zaidi na kuweka jitihada katika masomo na vipaji vyao kwa ujumla. Tunapenda kuona tuzo hizi zikiendelea kukua na kuwa kubwa zaidi kila mwaka,” amesema Dkt. Makoye.Aliongeza kuwa TaSUBa itaendelea kuboresha mfumo wa tuzo hizo ili ziwe chachu ya ushindani wenye tija, ubunifu na maendeleo ya tasnia ya sanaa nchini.TaSUBa Awards zimeendelea kuwa moja ya matukio muhimu chuoni, zikitoa fursa ya kutambua na kuthamini vipaji vya wanafunzi pamoja na kuwahamasisha kuendelea kujifunza, kubuni na kufanya kazi kwa weledi katika sekta ya sanaa na utamaduni.
Kaole Road
Anuani ya posta: P.O.BOX 32 Bagamoyo Tanzania
Simu: +255 762544613
Simu ya kiganjani: +255 766 264 581
Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas
Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.