• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania WIZARA YA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Huduma Zetu
    • Kikundi cha Bagamoyo
    • Vyumba vya Mikutano
    • Ushauri
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Ofisi
    • Vitengo
  • Taaluma
    • Kozi Zitolewazo
    • Fomu za Maombi
    • Matokeo ya Mtihani
  • Tamasha la Bagamoyo
    • Kuhusu Tamasha
    • Tamasha la 41
    • Fomu za Maombi ya Tamasha
    • Tamasha la 40
    • Tamasha la 39
    • Tamasha la 38
  • Kituo cha habari
    • TaSUBa TV
    • Maktaba ya Picha
  • Wasiliana
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Majarida
    • Vipeperushi
    • Taarifa kwa umma

BODI YA USHAURI TaSUBa YAANZA KAZI RASMI

Posted on: July 7th, 2022

BODI ya Ushauri (MAB) ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) imefanya kikao chake cha kwanza Julai 06, chini ya mwenyekiti wake Bw. George Yambesi ambaye ni Katibu Mkuu Mstaafu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Bw. Yambesi ametoa shukrani kwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa kwa kuwaamini na kuwateua kuwa wajumbe wa bodi hiyo.

“Tunamshukuru Waziri kwa uteuzi huu na tunaahidi kufanya kazi kwa weledi na nguvu zote ili kuleta tija na ufanisi katika kuijenga TaSUBa,” amesema Yambesi.

Vile vile Bw. Yambesi amemshukuru Mkuu wa Chuo Dkt. Herbert Makoye na menejimenti yote kwa mapokezi mazuri waliyowapa na kuahidi ushirikiano kwa uongozi wa chuo pamoja na wadau wengine wa sanaa.

Mwenyekiti Yambesi amewapongeza pia wajumbe wote wa bodi kwa kuteuliwa na kuwa sehemu katika mchango wa kuleta tija katika chuo hicho cha sanaa chenye ubora uliotukuka Afrika Mashariki katika kutoa mafunzo ya sanaa na utamaduni.    

Naye Mkuu wa Chuo Dkt. Herbert Makoye kwa niaba ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, ameipongeza Bodi na kuwashukuru wajumbe kwa kukubali uteuzi huo.

“Menejimenti tuko tayari kufanya kazi na kutekeleza maelekezo ya bodi kwa kufanya kazi pamoja ili kufikia malengo yaliyofanya Serikali ifungue chuo hiki,” amesema Dkt. Makoye.   

Wajumbe wa Bodi hiyo ambao ni Prof. Omary Halfa Mbura, Bw. Haruni Benge Matagane, Dkt. Elizabeth Godwin Mahenge na Dkt. Emmanuel Mwesiga Ishengoma,  waliteuliwa na Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa Machi 25, 2025.   

Matangazo

  • STUDENTS SELECTED MARCH INTAKE 2023 March 23, 2023
  • JOINING INSTRUCTION FOR MARCH INTAKE 2023 March 23, 2023
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA BUNGE YAPONGEZA TaSUBa KWA KUZALISHA WATAALAM MAHIRI WA SANAA NA UTAMADUNI

    March 18, 2023
  • SERIKALI KUENDELEA KUIBORESHA TAASISI YA SANAA - BAGAMOYO

    March 15, 2023
  • UDAHILI UMEFUNGULIWA MACHI INTAKE

    February 08, 2023
  • NAIBU WAZIRI GEKUL AIPONGEZA TaSUBa KWA USIMAMIZI MZURI WA RASILIMALI FEDHA PAMOJA NA KUWEKA HISTORIA YA UDAHILI MKUBWA

    December 01, 2022
  • Angalia zote

Video

Sanaa Tuition fee waiver scholarship
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Sanaa la Taifa
  • Dirisha la Hati ya Mshahara
  • Dirisha la Watumishi

Viunganishi Linganifu

  • WIZARA YA UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Kaole Road

    Anuani ya posta: P.O.Box 32 Bagamoyo Tanzania

    Simu: +255 023 2440149

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas

Other Contacts

   

Idadi ya waliotembelea Tovuti

Counter Widgets

    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Copyright ©2022 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.