• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • NeST |
    • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS)) |
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Huduma Zetu
    • Kikundi cha Bagamoyo
    • Vyumba vya Mikutano
    • Ushauri
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Ofisi
    • Vitengo
  • Taaluma
    • Kozi Zitolewazo
    • Fomu za Maombi
    • Matokeo ya Mtihani
    • Prospectus
  • Tamasha la Bagamoyo
    • Kuhusu Tamasha
    • Mwongozo wa Tamasha
    • Fomu za Maombi ya Tamasha
    • Tamasha la 43
    • Tamasha la 42
    • Tamasha la 41
    • Tamasha la 40
    • Tamasha la 39
    • Tamasha la 38
  • Kituo cha habari
    • TaSUBa TV
    • Maktaba ya Picha
  • Wasiliana
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Majarida
    • Vipeperushi
    • Taarifa kwa umma

Serikali: TaSUBa itaendelea kuwa kituo bora cha Mafunzo ya Sanaa na Utamaduni

Posted on: December 17th, 2021

Naibu Waziri, Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Pauline Gekul ameipongeza Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kutoa mafunzo na malezi katika kukuza taaluma ya sanaa na utamaduni ambayo ni muhimu kwa maendeleo ya jamii yoyote duniani. 

Mhe. Gekul ambae alikua mgeni rasmi katika mahafali ya 32 ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) yaliyofanyika Disemba 17, 2021 katika ukumbi wa Taasisi ya Sanaa Bagamoyo, alisema Serikali inatambua umuhimu wa sanaa na utamaduni ndio maana kupitia wizara ya  Utamaduni, Sanaa na Michezo imeweka sera ya kusimamia utamaduni kwa ujumla na sanaa ikiwepo ndani yake.

 

“Taasisi hii ni ya pekee nchini mwetu na ukanda wa Afrika Mashariki inayotoa mafunzo ya sanaa kwa kiwango cha astashahada na stashahada, basi kuna umuhimu mkubwa wa kuboresha zaidi taaluma hii ili iendane na mazingira ya dunia ya sasa ya utandawazi,” alisema Mhe. Gekul.

Mhe. Naibu Waziri aliwashukuru wasanii (wanachuo) kwa maonyesho ya sanaa ikiwa ni sehemu ya shughuli muhimu zinazofanywa na Taasisi hiyo pamoja na wasanii wengine. “Hakika ni kazi nzuri zinazoonyesha umuhimu wa sanaa kwa maendeleo ya nchi yetu,” alisema Mhe. Gegul.

Mhe. Gekul amesema Serikali itashirikiana na wadau mbalimbali wa sanaa kuhakikisha TaSUBa inaendelea kua kituo bora cha mafunzo ya sanaa na utamaduni nchini na afrika kwa ujumla. 

Jumla ya wahitimu waliotunukiwa vyeti ni 252 ambapo wahitimu wa Astashahada ni 150 (Me 118 na ke 32) na wa Stashahada ni 102 (Me 75 na ke 27).

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA NA CHUO INGIZO LA MACHI KWA MWAKA WA MASOMO 2025-2026 December 03, 2024
  • JOIN INSTRUCTION KWA MWAKA WA MASOMO 2025/2026 April 02, 2025
  • Call for the artists Bagamoyo Festival - 2025 May 05, 2025
  • Wito kwa wasanii Tamasha la Bagamoyo - 2025 May 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    March 04, 2025
  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    December 19, 2024
  • *SERIKALI KUENDELEA KUFANYA UWEKEZAJI MKUBWA TaSUBa*

    December 07, 2024
  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    December 03, 2024
  • Angalia zote

Video

KARIBU JIUNGE NA CHUO TaSUBa KWA MUHULA WA MACHI 2025
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS))
  • Dirisha la Hati ya Mshahara
  • Baraza la Sanaa la Taifa

Viunganishi Linganifu

  • WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Kaole Road

    Anuani ya posta: P.O.BOX 32 Bagamoyo Tanzania

    Simu: +255 762544613

    Simu ya kiganjani: +255 766 264 581

    Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas

Other Contacts

   

Idadi ya waliotembelea Tovuti

Counter Widgets

    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.