• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania WIZARA YA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Huduma Zetu
    • Kikundi cha Bagamoyo
    • Vyumba vya Mikutano
    • Ushauri
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Ofisi
    • Vitengo
  • Taaluma
    • Kozi Zitolewazo
    • Fomu za Maombi
    • Matokeo ya Mtihani
  • Tamasha
    • Kuhusu Tamasha
    • Tamasha la 41
    • Fomu za Maombi ya Tamasha
  • Kituo cha habari
    • TaSUBa TV
    • Maktaba ya Picha
  • Wasiliana
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Majarida
    • Vipeperushi
    • Taarifa kwa umma

MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE AFUNGA TAMASHA LA KIMATAIFA LA 40 LA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO

Posted on: October 30th, 2021

Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amesema Tamasha la 40 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni la Bagamoyo lililomalizika Oktoba 30, 2021 mjini Bagamoyo limetia fora kutokana na uratibu mzuri uliofanywa na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo pamoja na wadau wengine.

Mhe Kikwete ameyasema hayo Oktoba 30, 2021 wakati akifunga Tamasha hilo ambapo amesisitiza kuwa limeunga mkono jitihada za Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan za kutangaza utamaduni wa Tanzania ambapo pia amepongeza kwa kushirikisha mataifa mbalimbali na kulifanya kuwa la kihistoria na kimataifa zaidi.

 

Amefafanua kwamba, hivi karibuni Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan aliandaa filamu ya Royal Tour iliyohusisha ziara kwenye mji wa Bagamoyo kwa ajili ya kutangaza utamaduni wa mtanzania.

Pia, amesifu uratibu wa siku ya mwisho la Tamasha la Kimataifa la Bagamoyo wa kuandaa ziara iliyoongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo. Dkt, Hassan Abbasi na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Zainabu Abdallah, iliyoitwa jina la “Bagamoyo Royal Tour” iliyowajumuisha wasanii wa fani mbalimbali kama vile muziki, filamu, sanaa za ufundi, urembo na waandishi wa habari kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii katika mji wa Bagamoyo na baadaye mbuga ya Saadan.

Aidha, Mhe. Kikwete ameipongeza Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, kutumia Tamasha hili kwa kutoa huduma ya wachanjo ya Uviko -19 pamoja na kutoa ushauri na  kupima UKIMWI kwa hiari.

Katika Tamasha hilo Mhe. Kikwete amefafanua umuhimu wa sekta hizi kwa Taifa letu ambapo amesema kutokana na umuhimu wa Sekta za Utamaduni, Sanaa na Michezo, haijawahi kutokea kuachwa kuundiwa Wizara katika awamu zote toka enzi ya Serikali ya Awamu ya Kwanza ya Mwalimu Nyerere na kwamba kutokana na umuhimu huo Rais Samia ameendelea kuzibakiza na kuiziboresha.

Ameipongeza Wizara kwa kuendelea kuboresha sekta za Sanaa na Utamaduni kupitia taasisi zake za Bodi ya Filamu, COSOTA, BASATA na BAKITA na kuzitaka ziendelee kusimamia na kusaidia kazi za Wasanii ili waweze kunufaika nazo.

Aidha Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Pauline Gekul ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwapa moyo Wizara kuendeleza Tamasha hilo lenye historia katika Taifa la Tanzania.

Amefafanua kuwa Tamasha hili ndiyo Tamasha kongwe zaidi nchini na limebeba historia ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo ambayo zamani ilikua ikijulikana kama Chuo cha Sanaa Bagamoyo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuthamini mchango wa Tamasha hili ambapo ameahidi kuendelea kushirikiana na Wizara kuboresha Tamasha hilo ambalo amesisitiza kuwa lina faida kubwa siyo tu kwa wakazi wa Bagamoyo bali kwa taifa zima.

Matangazo

  • MAOMBI YA KUJIUNGA NA CHUO KWA MWAKA WA MASOMO 2022/2023 April 19, 2022
  • APPLICATION FORM FOR ADMISSION TO CERTIFICATE AND DIPLOMA PROGRAMMES FOR ACADEMIC YEAR 2022/2023 April 19, 2022
  • WITO KWA WASANII KUSHIRIKI KATIKA TAMASHA LA 41 LA KIMATAIFA LA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO KUANZIA TAREHE 22 HADI 29 OKTOBA 2022 April 01, 2022
  • JOINING INSTRUCTION TO JOIN Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) SEPTEMBER 2021 September 21, 2021
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TaSUBa YAENDESHA KAMPENI YA ELIMU KUHUSU MADHARA YA MIMBA ZA UTOTONI NA UMUHIMU WA ELIMU KWA MABINTI

    May 16, 2022
  • Mchengerwa: Serikali Kuboresha Sekta ya Filamu Nchini

    April 09, 2022
  • WAZIRI MCHENGERWA: TaSUBa Taasisi ya Kimkakati

    February 12, 2022
  • Serikali: TaSUBa itaendelea kuwa kituo bora cha Mafunzo ya Sanaa na Utamaduni

    December 17, 2021
  • Angalia zote

Video

Sanaa Tuition fee waiver scholarship
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Sanaa la Taifa
  • Dirisha la Hati ya Mshahara
  • Dirisha la Watumishi

Viunganishi Linganifu

  • WIZARA YA UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Kaole Road

    Anuani ya posta: P.O.Box 32 Bagamoyo Tanzania

    Simu: +255 023 2440149

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas

Other Contacts

   

Idadi ya waliotembelea Tovuti

Counter Widgets

    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Copyright ©2022 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.