Mhitimu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa), Karim Swafi, ameendelea kuonyesha uwezo mkubwa wa vijana wa Kitanzania katika medani za kimataifa baada ya kuipeperusha bendera ya Tanzania katika mashindano ya Yogasana yaliyofanyika jijini Ahmedabad, India, na kufanikiwa kujishindia tuzo nne.Mafanikio hayo yameiweka Tanzania katika ramani ya kimataifa ya mchezo na sanaa ya Yogasana, huku yakionesha matokeo chanya ya uwekezaji katika elimu ya sanaa na maendeleo ya vipaji vya vijana. Karim alionesha umahiri, nidhamu na ubunifu wa hali ya juu katika mashindano hayo yaliyowakutanisha washiriki kutoka mataifa mbalimbali duniani.Mafanikio ya Karim Swafi yanaendelea kuthibitisha kuwa TaSUBa ni kitovu cha kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vinavyoweza kushindana na kufanya vizuri katika ngazi za kitaifa na kimataifa.
Kaole Road
Anuani ya posta: P.O.BOX 32 Bagamoyo Tanzania
Simu: +255 762544613
Simu ya kiganjani: +255 766 264 581
Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas
Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.