• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • NeST |
    • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS)) |
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Huduma Zetu
    • Kikundi cha Bagamoyo
    • Vyumba vya Mikutano
    • Ushauri
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Ofisi
    • Vitengo
  • Taaluma
    • Kozi Zitolewazo
    • Fomu za Maombi
    • Matokeo ya Mtihani
    • Prospectus
  • Tamasha la Bagamoyo
    • Kuhusu Tamasha
    • Mwongozo wa Tamasha
    • Fomu za Maombi ya Tamasha
    • Tamasha la 43
    • Tamasha la 42
    • Tamasha la 41
    • Tamasha la 40
    • Tamasha la 39
    • Tamasha la 38
  • Kituo cha habari
    • TaSUBa TV
    • Maktaba ya Picha
  • Wasiliana
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Majarida
    • Vipeperushi
    • Taarifa kwa umma

TASUBA YATIA SAINI MAKUBALIANO NA CHUO CHA TAALUMA YA UREKEBISHAJI TANZANIA (TCTA)

Posted on: June 2nd, 2021

Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) imeingia makubaliano ya ushirikiano katika kuendesha Mafunzo ya Kozi za Sanaa na Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania (TCTA).

Makubaliano hayo ambayo yamesainiwa Ukonga katika Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania  na wakuu wa Taasisi hizo mbili ambao ni Bw. Gabriel Kiiza, Kaimu Mkuu wa Chuo TaSUBa na Kamishna Msaidizi wa Magereza Joe Gideon Matani, Mkuu wa Chuo TCTA, wamekubaliana kwamba TaSUBa kwa kushirikiana na TCTA wataandaa na kutoa mafunzo ya kozi za sanaa katika maeneo ya muziki, uigizaji na Ngoma; pia mafunzo yatakuwa yanatolewa kwa kipindi cha muda mfupi (Short Courses) kwa kipindi kisichopungua mwezi moja na kisichozidi miezi mitatu kwa kila udhahili. Aidha mafunzo yatatolewa na kuendeshwa katika madarasa ya TCTA ambapo maktaba pamoja na vifaa vya kujifunzia vitakuwa vya TCTA na endapo TCTA itakuwa na uhaba wa vifaa vya mafunzo, vitaazimwa kutoka TaSUBa kama vitakwepo vyakutosheleza.

Vile vile, bila kuathiri Ibara ya 3(a) ya Makubaliano hayo, TCTA itakuwa na wajibu wa kuwasafirisha wanafunzi na kuwapeleka TaSUBa kabla ya kuhitimu mafunzo angalau mara moja kwa kila udhahili ili kuweza kujifunza mazingira ya TaSUBa.

Awali kabla ya utiaji saini wa makubaliano hayo, Mkuu wa Chuo TCTA, Kamishna Msaidizi wa Magereza Joe Gideon Matani alisema, utiaji saini wa makubaliano hayo lilikua jambo la maandalizi la muda mrefu lakini sasa anafarijika kwa kuwa limekamilika na sasa kazi iendelee.

Mashirikiano hayo yatakua ni fursa nzuri ya kupeana uzoefu katika mafunzo hayo ya Sanaa na Utamaduni kwa kuwa TaSUBa wamebobea na wana uzoefu katika utoaji wa mafunzo ya Sanaa na Utamaduni kwa miaka mingi.

Awali chuo hicho kilikua kikitoa mafunzo kwa askari tu lakini sasa wamepanua wigo na kinatoa mafunzo kwa askari na raia.

Matangazo

  • FOMU YA KUJIUNGA NA CHUO KWA MWAKA WA MASOMO 2025-2026 SEPTEMBER INTAKE May 28, 2025
  • JOIN INSTRUCTION KWA MWAKA WA MASOMO 2025/2026 April 02, 2025
  • Call for the artists Bagamoyo Festival - 2025 May 05, 2025
  • Wito kwa wasanii Tamasha la Bagamoyo - 2025 May 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KARIBU UJIUNGE NA KOZI YA MUDA MFUPI YA MUZIKI

    May 29, 2025
  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    March 04, 2025
  • JIUNGE NA CHUO INGIZO LA MACHI 2025

    December 19, 2024
  • *SERIKALI KUENDELEA KUFANYA UWEKEZAJI MKUBWA TaSUBa*

    December 07, 2024
  • Angalia zote

Video

KARIBU JIUNGE NA CHUO TaSUBa KWA MUHULA WA MACHI 2025
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS))
  • Dirisha la Hati ya Mshahara
  • Baraza la Sanaa la Taifa

Viunganishi Linganifu

  • WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Kaole Road

    Anuani ya posta: P.O.BOX 32 Bagamoyo Tanzania

    Simu: +255 762544613

    Simu ya kiganjani: +255 766 264 581

    Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas

Other Contacts

   

Idadi ya waliotembelea Tovuti

Counter Widgets

    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.