Mhitimu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa), Stellabeatrice Dominic, amewataka vijana kujenga misingi imara ya taaluma zao mapema ili kuongeza nafasi za kupata fursa mbalimbali za ajira na ushirikiano wa kikazi wanapoingia kwenye soko la ajira.Akizungumza kuhusu safari yake ya taaluma, Stellabeatrice amesema ni muhimu kwa vijana kuanza kutafuta na kutumia fursa zinazohusiana na taaluma wanazosomea wakiwa bado chuoni, kwani hatua hiyo huwasaidia kujenga mtandao wa mahusiano ya kikazi (networking), kupata uzoefu wa vitendo na kujitangaza kupitia kazi wanazozifanya.Ameeleza kuwa kujihusisha na shughuli za kitaaluma mapema kunawapa wanafunzi nafasi ya kutambulika katika tasnia husika kabla hata ya kuhitimu masomo yao, jambo ambalo huwapa urahisi wa kupata kazi au miradi wanapoingia rasmi kwenye mazingira ya kazi.“Vijana wasisubiri kuhitimu ndipo waanze kutafuta fursa. Waanze mapema wakiwa chuoni kwa kushiriki miradi, mafunzo ya vitendo na kujenga mahusiano na wadau wa sekta husika. Hii itawasaidia kuendana na mahitaji ya soko la ajira na kuongeza ushindani wao,” amesema Stellabeatrice.
Kaole Road
Anuani ya posta: P.O.BOX 32 Bagamoyo Tanzania
Simu: +255 762544613
Simu ya kiganjani: +255 766 264 581
Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas
Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.