• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • NeST |
    • Dirisha la Watumishi (Employee Self Service (ESS)) |
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)
TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Huduma Zetu
    • Kikundi cha Bagamoyo
    • Vyumba vya Mikutano
    • Ushauri
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Ofisi
    • Vitengo
  • Taaluma
    • Kozi Zitolewazo
    • Fomu za Maombi
    • Matokeo ya Mtihani
    • Prospectus
  • Tamasha la Bagamoyo
    • Tamasha la 44
    • Tamasha la 43
    • Tamasha la 42
    • Tamasha la 41
    • Tamasha la 40
    • Tamasha la 39
    • Tamasha la 38
  • Kituo cha habari
    • TaSUBa TV
    • Maktaba ya Picha
  • Wasiliana
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Majarida
    • Vipeperushi
    • Taarifa kwa umma

Video

  • TaSUBa YASHIRIKI MAZOEZI YA YOGA KWA AJILI YA KUIMARISHA AFYA

    June 15th, 2026

    WANAFUNZI na watumishi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) leo wameshiriki mazoezi ya yoga yaliyofanyika katika viwanja vya Taasisi hiyo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya 12 ya Kimataifa ya Yoga yanayotarajiwa kufanyika hivi karibuni.Mazoezi hayo yaliandaliwa na Kituo cha Utamaduni cha Watu wa India kwa lengo la kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa yoga katika kuimarisha afya ya mwili, akili na ustawi wa maisha kwa ujumla.Washiriki walipata fursa ya kujifunza na kufanya mazoezi mbalimbali ya yoga chini ya uongozi wa wataalamu, huku wakielezwa manufaa ya yoga katika kupunguza msongo wa mawazo, kuongeza umakini na kuboresha afya ya mwili.Akizungumza wakati wa shughuli hiyo, mmoja wa waandaaji alieleza kuwa yoga ni nyenzo muhimu ya kujenga afya bora na kuimarisha mahusiano ya kijamii kupitia mazoezi yanayowaleta watu pamoja bila kujali tofauti zao.Kwa upande wake, TaSUBa imeendelea kuonesha ushirikiano wake katika shughuli zinazochangia maendeleo ya sanaa, utamaduni na ustawi wa jamii kwa kushiriki kikamilifu katika mazoezi hayo. Ushiriki huo pia umeonesha dhamira ya taasisi katika kuhamasisha mtindo bora wa maisha unaojumuisha afya ya mwili na akili.Maadhimisho ya Kimataifa ya Yoga huadhimishwa duniani kote kila mwaka kwa lengo la kuhamasisha matumizi ya yoga kama njia ya kuimarisha afya, amani na mshikamano miongoni mwa watu wa mataifa mbalimbali.

  • MTANZANIA AIPEPERUSHA BENDERA YA TANZANIA NCHINI INDIA

    June 13th, 2026

    Mhitimu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa), Karim Swafi, ameendelea kuonyesha uwezo mkubwa wa vijana wa Kitanzania katika medani za kimataifa baada ya kuipeperusha bendera ya Tanzania katika mashindano ya Yogasana yaliyofanyika jijini Ahmedabad, India, na kufanikiwa kujishindia tuzo nne.Mafanikio hayo yameiweka Tanzania katika ramani ya kimataifa ya mchezo na sanaa ya Yogasana, huku yakionesha matokeo chanya ya uwekezaji katika elimu ya sanaa na maendeleo ya vipaji vya vijana. Karim alionesha umahiri, nidhamu na ubunifu wa hali ya juu katika mashindano hayo yaliyowakutanisha washiriki kutoka mataifa mbalimbali duniani.Mafanikio ya Karim Swafi yanaendelea kuthibitisha kuwa TaSUBa ni kitovu cha kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vinavyoweza kushindana na kufanya vizuri katika ngazi za kitaifa na kimataifa.

  • TaSUBa KITUO CHA KUIBUA WATAYARISHAJI NA WATAALAMU WA MUZIKI WA KISASA

    June 11th, 2026

    Katika ulimwengu wa muziki unaoendelea kukua kwa kasi, hitaji la wataalamu wenye ujuzi wa utayarishaji wa muziki wa kisasa limeongezeka zaidi kuliko wakati mwingine wowote. Chuo cha Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kinaendelea kuwa kitovu cha kuibua vipaji na kuzalisha wataalamu wa muziki wanaoweza kushindana katika soko la ajira na tasnia ya ubunifu ndani na nje ya Tanzania.Kupitia mafunzo ya kitaalamu yanayojumuisha matumizi ya teknolojia za kisasa za sauti, utayarishaji wa muziki, uandishi wa nyimbo, pamoja na mbinu mbalimbali za uzalishaji wa kazi za muziki, wanafunzi hupata maarifa na ujuzi unaowajengea msingi imara wa mafanikio katika sekta ya muziki.

  • ← Prev
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • Next →

Matangazo

  • SELECTED APPLICANTS MARCH INTAKE 2026 March 31, 2026
  • FOMU YA KOZI FUPI July 14, 2025
  • FOMU YA KUJIUNGA NA CHUO MWAKA WA MASOMO 2025/2026 August 18, 2025
  • ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA TaSUBa SEPTEMBER INTAKE 2024 August 05, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TaSUBa TUTASHIRIKI WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2026

    June 14, 2026
  • MTANZANIA AIPEPERUSHA BENDERA YA TANZANIA NCHINI INDIA

    June 13, 2026
  • TaSUBa KITUO CHA KUIBUA WATAYARISHAJI NA WATAALAMU WA MUZIKI WA KISASA

    June 11, 2026
  • Mfumo wa e -MREJESHO Hurahishisha Mawasiliano ya Serikali na Wananchi

    June 09, 2026
  • Angalia zote

Video

NIDHAMU NI MSINGI WA MAFANIKIO KWA MSANII
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

Viunganishi Linganifu

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

Idadi ya waliotembelea Tovuti

Counter Widgets

    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.