Mmoja wa waalimu katika Idara ya Ngoma na Sarakasi ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa), Bw. Epimack Luanda, amesema kuwa sanaa bila elimu ni vigumu kwa msanii kutoa kazi zitakazoweza kushindana katika soko la ndani na la nje ya nchi.Mwalimu Epimack amewataka wasanii na vijana wenye vipaji kujitokeza kujiunga na Taasisi hiyo ili kupata elimu ya kitaalamu itakayowasaidia kukuza vipaji vyao.Akizungumza kuhusu umuhimu wa elimu katika sanaa, Bw. Luanda amesema TaSUBa huwapa wanafunzi nafasi ya kujifunza aina mbalimbali za sanaa pamoja na maarifa muhimu ya uongozi, masoko na ujasiriamali wa sanaa ili waweze kujitegemea na kufanya kazi kwa ubunifu na weledi zaidi.
Nguli wa zamani wa timu ya Taifa ya England na Klabu ya Manchester United Rio Ferdinand awasili nchini na kupokelewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Makonda.
Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.