Nafasi za kujiunga na Chuo - TaSUBa kwa ingizo la Septemba.
Usikose fursa hii adhimu ya kuitendea ipasavyo "talent" yako.
Jiunge na Chuo TaSUBA upate elimu bora, maarifa ya vitendo katika kukuza kipaji chako.
Tuma maombi yako sasa kujiunga na Chuo chenye mazingira bora ya kujifunzia katika kujenga "future" yako.
Wasiliana nasi: +255 762 544 613 / +255 766 264 581
WATAALAMU wa afya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani ya Tumbi wamefika katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kwa lengo la kutoa elimu na kuhamasisha uchangiaji wa damu salama.Katika zoezi hilo, wataalamu hao wa afya walieleza umuhimu wa kuchangia damu kwa hiari, wakibainisha kuwa damu ni muhimu katika kuokoa maisha ya wagonjwa wanaohitaji huduma za dharura, wajawazito, watoto pamoja na watu wanaopata ajali.Aidha, walitoa wito kwa watumishi na wanafunzi wa TaSUBa kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la uchangiaji damu, wakisisitiza kuwa tendo hilo ni la kibinadamu na lina mchango mkubwa katika kusaidia jamii.
Mmoja wa waalimu katika Idara ya Ngoma na Sarakasi ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa), Bw. Epimack Luanda, amesema kuwa sanaa bila elimu ni vigumu kwa msanii kutoa kazi zitakazoweza kushindana katika soko la ndani na la nje ya nchi.Mwalimu Epimack amewataka wasanii na vijana wenye vipaji kujitokeza kujiunga na Taasisi hiyo ili kupata elimu ya kitaalamu itakayowasaidia kukuza vipaji vyao.Akizungumza kuhusu umuhimu wa elimu katika sanaa, Bw. Luanda amesema TaSUBa huwapa wanafunzi nafasi ya kujifunza aina mbalimbali za sanaa pamoja na maarifa muhimu ya uongozi, masoko na ujasiriamali wa sanaa ili waweze kujitegemea na kufanya kazi kwa ubunifu na weledi zaidi.
Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.