Mkazi wa Bagamoyo, Bw. Shabani Ramadhani, ameeleza kuwa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) imekuwa na mchango mkubwa katika kukuza, kuendeleza na kutangaza sanaa nchini Tanzania kwa miaka mingi.Amesema uwepo wa TaSUBa umeiwezesha Bagamoyo kuwa kitovu muhimu cha sanaa na utamaduni, huku ikitoa fursa kwa vijana wengi kupata elimu ya sanaa na kuendeleza vipaji vyao katika nyanja mbalimbali za ubunifu.Bw. Ramadhani pia amepongeza Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, akieleza kuwa tamasha hilo limekuwa jukwaa muhimu linalowakutanisha wasanii kutoka Tanzania na mataifa mbalimbali duniani kwa ajili ya kubadilishana uzoefu, kuonesha kazi zao na kuimarisha ushirikiano wa kiutamaduni.
Mwalimu Felix Sesoa ambaye ni mkufunzi katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) anaeleza kuwa teknolojia ya majukwaa (Stage Technology) ni sehemu muhimu katika mafanikio ya maonesho yoyote ya sanaa, kwani huchangia kwa kiasi kikubwa ubora wa uwasilishaji wa kazi za wasanii kwa hadhira.Anaeleza kuwa teknolojia ya majukwaa inahusisha matumizi ya vifaa na mifumo mbalimbali ya taa, sauti, mapambo ya jukwaa, pamoja na mbinu za kiufundi zinazowezesha maonesho kufanyika kwa ufanisi na kuvutia watazamaji."Hata kama wasanii wana vipaji vikubwa, maonesho yao yanaweza kupungua thamani endapo hayatasaidiwa na teknolojia bora ya jukwaani," anasema Mwl. Sesoa.
Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt. Herbert Makoye ametoa wito kwa vijana kujitokeza kwa wingi kuchangia damu salama ili kusaidia kuokoa maisha ya wagonjwa wenye uhitaji wa damu katika hospitali mbalimbali nchini.Amesema vijana wana nafasi kubwa ya kusaidia jamii kupitia uchangiaji wa damu kwani kitendo hicho ni salama na chenye manufaa makubwa kwa wagonjwa wanaohitaji huduma za dharura, wajawazito pamoja na watoto.
Kaole Road
Anuani ya posta: P.O.BOX 32 Bagamoyo Tanzania
Simu: +255 762544613
Simu ya kiganjani: +255 766 264 581
Barua pepe: application@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu masomo) info@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo ya ujumla) bagamoyofest@tasuba.ac.tz (Barua pepe hii inatumika kwenye mambo yote yanayohusu Tamasha) tas
Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.