Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt. Herbert Makoye ametoa wito kwa vijana kujitokeza kwa wingi kuchangia damu salama ili kusaidia kuokoa maisha ya wagonjwa wenye uhitaji wa damu katika hospitali mbalimbali nchini.Amesema vijana wana nafasi kubwa ya kusaidia jamii kupitia uchangiaji wa damu kwani kitendo hicho ni salama na chenye manufaa makubwa kwa wagonjwa wanaohitaji huduma za dharura, wajawazito pamoja na watoto.
Nafasi za kujiunga na Chuo - TaSUBa kwa ingizo la Septemba.
Usikose fursa hii adhimu ya kuitendea ipasavyo "talent" yako.
Jiunge na Chuo TaSUBA upate elimu bora, maarifa ya vitendo katika kukuza kipaji chako.
Tuma maombi yako sasa kujiunga na Chuo chenye mazingira bora ya kujifunzia katika kujenga "future" yako.
Wasiliana nasi: +255 762 544 613 / +255 766 264 581
WATAALAMU wa afya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani ya Tumbi wamefika katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kwa lengo la kutoa elimu na kuhamasisha uchangiaji wa damu salama.Katika zoezi hilo, wataalamu hao wa afya walieleza umuhimu wa kuchangia damu kwa hiari, wakibainisha kuwa damu ni muhimu katika kuokoa maisha ya wagonjwa wanaohitaji huduma za dharura, wajawazito, watoto pamoja na watu wanaopata ajali.Aidha, walitoa wito kwa watumishi na wanafunzi wa TaSUBa kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la uchangiaji damu, wakisisitiza kuwa tendo hilo ni la kibinadamu na lina mchango mkubwa katika kusaidia jamii.
Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.